Вход на сайт

Просмотр новости

Найдите то, что Вас интересует

Hispania yaivua Argentina ubingwa wa Dunia

Дата публикации: 19-07-2026 22:17:04

Dakika 90 za mchezo huo zilikamilika bila timu yoyote kufunga, huku Hispania ikiwa na udhibiti mkubwa wa mchezo na kutengeneza nafasi nyingi zaidi za kufunga.

Основное содержимое страницы с новостью.

Hispania imeandika historia mpya katika soka baada ya kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia 2026, ikiivua Argentina iliyokuwa bingwa mtetezi kwa ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliochezwa hadi dakika 120.

Shujaa wa La Roja alikuwa mshambuliaji Ferran Torres aliyefunga bao la ushindi dakika ya 106 kwa mguu wa kushoto, akimalizia pasi ya kichwa kutoka kwa Nico Williams na kuwapa Wahispania taji la pili la dunia.

Dakika 90 za mchezo huo zilikamilika bila timu yoyote kufunga, huku Hispania ikiwa na udhibiti mkubwa wa mchezo na kutengeneza nafasi nyingi zaidi za kufunga.

Hispania ilifanya mashambulizi 16 yaliyolenga lango la Argentina, huku 11 yakizuiwa na kipa Emiliano Martínez aliyekuwa nguzo muhimu kwa mabingwa hao wa zamani kwa kuokoa michomo hatari.

Kwa upande mwingine, Argentina ilishindwa kuonyesha makali kwenye safu yake ya ushambuliaji, ikicheza dakika zote 120 bila kupata shuti lililolenga lango.

Hispania ilikuwa ya kwanza kutishia lango dakika ya nne, baada ya mshambuliaji Lamine Yamal kupiga shuti lililozuiwa na mabeki wa Argentina kabla ya Martínez kuokoa hatari hiyo.

Argentina ilijibu dakika ya sita baada ya Lionel Messi kupata nafasi nzuri, lakini kipa Unai Simón alitoka kwa wakati na kumzuia mshambuliaji huyo asiingie kwenye eneo la kufunga.

Dakika ya 38, Mikel Oyarzabal alipata nafasi nzuri nje kidogo ya eneo la hatari, lakini shuti lake kali liliokolewa na Martínez.

Argentina ilipata pigo kabla ya kumalizika kwa mchezo baada ya kuwapoteza mabeki wake wawili, Lisandro Martínez na Cristian Romero, waliotoka kutokana na maumivu, lakini timu hiyo iliendelea kuonyesha nidhamu kubwa ya ulinzi.

Katika dakika za nyongeza, Argentina ilipata pigo lingine baada ya kiungo Enzo Fernández kuonyeshwa kadi nyekundu dakika ya 90+3 kufuatia kupata kadi mbili za njano ndani ya muda mfupi.

Ushindi huo umeifanya Hispania kutwaa Kombe la Dunia kwa mara ya pili katika historia yake, baada ya mafanikio ya kwanza mwaka 2010 kwenye fainali zilizofanyika Afrika Kusini, ambako pia ilishinda kwa bao 1-0.

Схожие новости

#Наименование новостиТональностьИнформативностьДата публикации
1Аргентина стала первой командой, не пробившей в створ ворот за 90 минут в финале ЧМ0519-07-2026
2Drámai végjáték, Spanyolország megállította Lionel Messit a foci-vb döntőjében5519-07-2026
3England, Argentina ilivyoingia kwenye mtego wa kisiasa0520-07-2026
4Испания выиграла ЧМ по футболу, обыграв Аргентину со счётом 1:05719-07-2026
5Испания победила Аргентину в финале чемпионата мира по футболу5719-07-2026
6Spagna campione del mondo. È la nazionale più titolata del XXI secolo5619-07-2026
7Аргентина и Испания не выявили победителя финала ЧМ-2026 в основное время0519-07-2026
8Spain is the 2026 World Cup champion, defeating Argentina for its 2nd title8719-07-2026
9Затянувшийся мастер‑класс: как Испания измучила Аргентину, довела до слёз Месси и во второй раз стала чемпионом мира0820-07-2026

Классификация: Спорт. Схожих патентов: 0. Схожих новостей: 9. Тональность: 0. Информативность: 5. Источник: www.mwananchi.co.tz.