Вход на сайт

Просмотр новости

Найдите то, что Вас интересует

Askofu Malasusa kuongoza ibada mazishi ya Mchungaji Silvanus

Дата публикации: 29-07-2026 07:22:06

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Alex Malasusa, leo Julai 29, 2026 anatarajiwa kuongoza ibada ya kuaga mwili wa Mchungaji Silvanus Msuya (44) katika Usharika wa Boko, Dayosisi ya Pwani na Mashariki, jijini Dar es Salaam, ambapo mamia ya waumini wa kanisa hilo watapata wasaa wa kushiriki ibada hiyo na kuaga mwili.

Основное содержимое страницы с новостью.

Moshi. Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Alex Malasusa, leo Julai 29, 2026 anatarajiwa kuongoza ibada ya kuaga mwili wa Mchungaji Silvanus Msuya (44) katika Usharika wa Boko, Dayosisi ya Pwani na Mashariki, jijini Dar es Salaam, ambapo mamia ya waumini wa kanisa hilo watapata wasaa wa kushiriki ibada hiyo na kuaga mwili.

Mchungaji Silvanus Msuya alifariki dunia Julai 26, 2026 katika Hospitali ya Rabininsia, jijini Dar es Salaam, alipokuwa amelazwa akisumbuliwa na nimonia kali. Ameacha mke na watoto watatu.

Novemba 3, 2024, Mchungaji Silvanus alibarikiwa kuwa mchungaji wa Dayosisi ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro, na amekuwa mchungaji kiongozi wa Usharika wa Spillway, Jimbo la Tambarare, mchungaji mwenza wa Usharika wa Kanisa Kuu Mwanga na Mratibu wa Habari na Mawasiliano wa Dayosisi ya Mwanga.

Akizungumza na Mwananchi, kaka wa marehemu, Elisa Msuya, amesema ibada ya kuaga mwili wa mpendwa wao itaanza saa mbili asubuhi leo Julai 29, 2026 katika Usharika wa Boko na kumalizika saa sita asubuhi.

Amesema baada ya taratibu zote za ibada na kuaga mwili wataanza safari kuelekea Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro, ambapo mwili wa Mchungaji Silvanus utapumzishwa nyumbani kwao katika Kijiji cha Shighatini kwa ajili ya taratibu za maziko.

Amesema kesho Julai 30, mwili wa mchungaji huyo utapelekwa katika Kanisa Kuu la KKKT Mwanga kwa ajili ya ibada ya mazishi, ambapo amesema taratibu zote za kiibada zitakapokamilika mwili utapelekwa katika Kanisa la Shighatini, ambapo ndipo mwili huo utakapozikwa.

"Mwili utakapofika Mwanga leo utapumzishwa Kijiji cha Shighatini, ambapo kesho asubuhi kuanzia saa 2 hadi saa 4 asubuhi kutakuwa na shughuli ya kuaga. Baada ya hapo kutakuwa na salamu mbalimbali na kuanzia saa 6 mchana kutakuwa na ibada ya mazishi, na baada ya hapo mwili wake utazikwa katika Kanisa la Shighatini," amesema kaka wa marehemu.

Схожие новости

#Наименование новостиТональностьИнформативностьДата публикации
1Masaju anavyoibua matarajio mhimili wa Mahakama01028-07-2026
2В Духовной столице Сибири молитвенно почтили память святителя Иоанна, митрополита Тобольского5724-06-2026
3Проповідь Блаженнішого Святослава до 100-ліття Мукачівської чудотворної ікони Богородиці 5524-06-2026
4Проповідь Блаженнішого Святослава у Понеділок Святого Духа 0001-06-2026
5Божественна Літургія з Патріаршого собору УГКЦ5321-06-2026
6La homilía de 30 de julio de 20250030-07-2025
7El Cascabel, 27 de julio de 2026031.8427-07-2026
8Pride of YLLSS: Illuminating Life Through Rectify Mind Cultivate Person024.2922-05-2026
9Слово Святейшего Патриарха Кирилла на встрече с преподавателями богословских курсов для монашествующих Валаамского монастыря0510-07-2026
10El Cascabel, 7 de julio de 2026031.8409-07-2026

Классификация: Культура. Схожих патентов: 0. Схожих новостей: 10. Тональность: 0. Информативность: 8.54. Источник: www.mwananchi.co.tz.